Kuikosoa Serikali siyo uhaini-Lissu. | bongo satellite.
Breaking News
Loading...

Monday, 29 August 2016

Kuikosoa Serikali siyo uhaini-Lissu.



Mwanasheria wa Mkuu Chadema, Tundu Lissu

Mwanasheria wa Mkuu Chadema, Tundu Lissu 
By Joster Mwangulumbi, Mwananchi; jmwangulumbi@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Mwanasheria wa Mkuu Chadema, Tundu Lissu amesema Katiba ya mwaka 1965 ilifuta vyama vingi ikabaki Tanu hali iliyoondoa uwezekano kikatiba wa kupinga au kukosoa utawala wa Awamu ya Kwanza bila kukabiliwa na nguvu za dola na kushtakiwa.
Lakini marekebisho ya mwaka 1992 yaliyotokana na Waraka Na 1 wa Serikali, yalirejesha mfumo wa vyama vingi ambamo ndani kuna uhuru na haki kisheria na kikatiba kuipinga na kuikosoa Serikali.
Mwanasheria huyo amesema kwa kuzingatia Katiba na Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992, kuipinga na kuikosoa Serikali si uhaini wala kosa kwani vyama vya upinzani vimepata uhalali huo kisheria na ndiyo maana vinasema haviwezi kuona Serikali ya Rais John Magufuli ikitumia mamlaka isiyokuwa nayo kwa kusigina Katiba na sheria.
Amesema tofauti kubwa kati ya utawala wa Mwalimu Nyerere na Rais Magufuli ni mamlaka waliyonayo kikatiba.
Mwananchi. 
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

0 comments:

POST A COMMENT