Siri hiyo imefichuliwa na Mbaga katika mahojiano maalumu na gazeti hili, ambaye amedai kuwa iwapo mabeki wa timu pinzani pamoja na waamuzi hawana umakini, ujanja wa Mrwanda utakuwa tatizo kwao.
“Nakumbuka mechi yangu ya kwanza kuchezesha Ligi Kuu ya Tanzania, ilikuwa ni kati ya AFC ya Arusha na Mtibwa. Hii ilikuwa lazima AFC ashinde ili abaki Ligi Kuu.
“Mchezo ulikuwa mzuri, dakika mbili za mwisho, Mrwanda alipata nafasi akabaki na beki anaitwa Godfrey Magoli wanakwenda katika lango la Mtibwa, Magoli akamshika Mrwanda na kumwachia.
Mwananchi.
Toa Maoni Hapa Chini
0 comments:
POST A COMMENT