
Wazazi wa raia mmoja wa Uingereza ambaye aliripotiwa kusafiri hadi nchini Iraq ili kujiunga na Kundi la Islamic State wamebaini kwamba walikamatwa na maafisa wa polisi.
John na Sally Letts walikiambia chombo cha habari cha Channel 4 kwamba walikamatwa baada ya kumtumia fedha za chakula na miwani mipya.

Maafisa wa polisi wa Thames Valley wamethibitisha kuwa iliwakamata wazazi hao.
Msemaji amesema kuwa :Mwanamume mmoja wa miaka 55 na mwanamke wa miaka 53 kutoka Oxford walikamatwa kwa tuhuma za kutuma fedha nchini Syria ambazo zitatumika kwa maswala ya kigaidi,na waliotolewa hadi februari 17.
Toa Maoni Hapa Chini
0 comments:
POST A COMMENT