Klabu ya Manchester City ya Uingereza imeepuka kukutana na meneja wake wa msimu ujao Pep Guardiola kwenye nusu fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Miamba hao wa Uingereza wamepwa Real Madrid ya Uhispania.
Bayern Munich wa Ujerumani, ambao kwa sasa wamo chini ya Pep Guardiola watakutana na Atlético Madrid ya Uhispania.
Mechi hizo zitachezwa 26/27 Aprili na 3/4 Mei.
Mpangilio huo natoa nafasi ya kuwepo debi ya Madrid fainali iwapo Atletico na Real zitafika fainali au hata kukutanisha Pep Guardiola na klabu yake ya msimu ujao fainali iwapo City na Bayern watafuzu.
Toa Maoni Hapa Chini
0 comments:
POST A COMMENT